VITU VITATU VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUPATA CONNECTION.



Ndugu yangu mwanamafanikio hongera sana kwa zawadi ya siku ya leo kutoka kwa muumba wetu maana hakuna zawadi iliyo kuu Zaidi ya uhai wako maana uhai ndio kitu pekee kinachofanya usome Makala hii, kwahiyo ndugu yangu hongera sana kwa zawadi ya leo.

Katika Makala ya leo nitakwenda kukuelekeza vitu vitatu ambavyo vitakusaidia kupata connection katika fursa mbalimbali, nachokuomba ni kuwa makini mwanzo a Makala hii mpaka mwisho.

Hatua ya kwanza;  KUJICONNECT.

Yaani hatua ya kwanza na ya msingi kuliko zote ni njia ya kujikonnect na kule unakotaka kupata konection mfano unaweza ukawa unataka kupata kazi katika ofisi  Fulani jaribu kujitolea kwenye ofisi hiyo yaani jaribu kujishusha sana  ndugu yangu ili kupata unachokitaka kwa lugha nyingine jipendekeze.

Hatua ya pili; FANYA KITU BORA BORA ZAIDI.

Unaweza  ukajikonnect lakini kama watu hawataona thamani yako ni lazima connection ipotee kwahiyo jaribu kufanya kitu bora ili watu waone ubora wako  na badae watakutengenezea connection sehemu tofauti tofauti na maanisha ukipata naasi itumie vizuri zaidi.

Hatua ya tatu; fanya  bila kuchoka(kuwa na usugu).

Haijarishi unapata matokeo gani kwa muda huo  unaotafuta connection, cha msingi wewe ni kufanya mpaka uone matokeo yaani unafanya kazi mpaka unaowafanyia kazi wanaona aibu na kukupa connection ya kile unachoitaji,

Asante sana rafiki yangu kwa kuwa nami katika Makala hii ya leo tukutane katika Makala zingine, leo ni kuache na Hizo  hatua ambazo unaweza kufata ukiwa unatafuta connectio mbalimbali.
Nakushauri kujaza fomu iliyopo ndani ya fikia lengo kuweza kutumiwa Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Aidan mponeza.
aidanmponeza@gmail.com


No comments

Powered by Blogger.