HII NDIO CHANGAMOTO KUBWA KULIKO ZOTE KWENYE MAISHA YAKO.
Ndugu yangu mpendwa wa mtandao wa fikia lengo, hongera kwa
kupata zawadi ya siku ya leo ni jambo la kumshukuru mungu sana kwa kutuamini na
siku ya leo kutupatia tena zawadi hii ya uzima.
Leo ndugu yangu nipende kukuuliza kwanini umepoteza
mwelekeo, kwanini umeanza kuishi ovyo ovyo bila mikakati ya kuishi, kwanini
unaanza kuwa na roho kukata tamaa, nakuuliza ndugu yangu kwanini umepunguza
kujiamini kisa changamoto ndogo kama hizo, ndio.! Nasema ndogo maana changamoto
kubwa ni moja tu duniani kukosa uhai.
Ndugu yangu haya yote unayopitia ni mapito yatapita ugumu
unaopitia wewe leo mimi niliuona toka kitambo na ndio maana kwenye ukurasa
wangu wa facebook nilikuambia ipo siku utabaki wewe na malengo yako basi.
Kuna muda ndugu yangu utaona wewe sio wa vile unavyotaka
kuwa kuna muda hakuna wa kukupa msaada juu ya malengo yako Zaidi yaw ewe na
malengo yako mwenyewe.
Nakuomba usipoteza mwelekeo, amini kule unataka kuwa ingali
unapitia nyakati za kukukatisha tamaa, wewe usikate yamaa songa mbele song
ahata kwa hatua ndogo lakini usipoteze mwelekeo.
Safari yako isisimame njiani yakupasa kusonga mbele bila
Kurudi nyuma nakuomba usonge mbele ndugu yangu, songa,songa usipoteze mwelekeo
nakutakia safari njema .
Unashauriwa kujaza taarifa zako katika fomu
hapo juu ili upate Makala katika email yako moja kwa moja nakuwa miongoni mwa
watu watakopokea zawadi ya kitabu kitakachotoka hivi karibuni asante sana.
instagram@Aidan_Mponeza
FACEBOOK@fikia lengo.
0762679204
email@aidanmponeza@gmail.com
FACEBOOK@fikia lengo.
0762679204
email@aidanmponeza@gmail.com
Leave a Comment