UMUHIMU WA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI NA MAKINI;
Ndugu yangu kuna msemo unasema hapo ulipo ni matokeo ya
maamuzi uliyofanya nyuma kwahiyo inaonyeha ni jinsi gani maamuzi yalivyo na
umuhimu katika maisha yetu na zifuatazo ni fanida ya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.
KWANZA;inaboresha maisha yako, kiukweli ubora wa maisha yako
ni matokeo ya maamuzi yako kwahiyo kama maisha yako ni bora basi maamuizi yako
yalikuwa ni bora pia.
PILI;inahamsha umakini wa hisia ,unapofanya maamuzi kwa
wakati sahihi unakua na hisia sahihi nakuziamini kwa maamuzi hayo.
TATu; inasaidia kumtafuta mungu katika hali, ni kweli
unapokuwa mshindi wa kitu sifa ni kwake mungu na mafanikio ya maamuzi yako
yanaweza kuwa ni chachu ya kuwa karibu na mungu.
NNE; inakupa uwezo wa kujiamini, uwezo wa kujiamini
unatokana na maamuzi uliyofanya na unayoendelea kufanya kama maamuzi yako ni
mabaya utapungukiwa na kujiamini mwenyewe nakuwa ni mtu wa kuomba ushauri kwa
kila maamuzi yako hata yale maamuzi ya kawaida.
Tano,inakufanya uishi maisha yako ya ndani, unaweza kuwa na
marafiki wengi ila mwenye uwezo wakufanya maamuzi yako ni wewe na unapofanya
maamuzi unakuwa na hisia za ndani ndo zinakusukuma.
SITA; inaondoa kujilaumu katika maamuzi uliyofanya na kuwa
na afya bora, kitendo cha kujilaumu tayari ni kujikataa na wewe na mwili wako
na inaweza ikawa chanzo cha malazi kama moyo na mengine hakika maamuzi sahihi
ni afya.
Ndugu hayo ndo muhimu na faida ya mafanikio lakini nikukumbushe
ya kuwa maamuzi bora yanaitaji muda na gharama ya hali kama ikiwezekana na mali
nikutakie siku njema na mungu akubariki karibu tena kwenye Makala zingine
asante na AIDAN MPONEZA
kama unaitaji ushauri au maoni karibu sana kwa rafiki yako aidan tuma sms anza na neno FIKIA.
SIMU NO;0 762679204,
EMAIL; fikialengo@gmail.com
www.fikialengo.blospot.com
kama unaitaji ushauri au maoni karibu sana kwa rafiki yako aidan tuma sms anza na neno FIKIA.
SIMU NO;0 762679204,
EMAIL; fikialengo@gmail.com
www.fikialengo.blospot.com
Leave a Comment