BARUA YA WAZI KWA WANAFUNZI NA WAHITIMU WA MASOMO YA UALIMU SAYANSI PAMOJA NA HISABATI.



Ndugu yangu  habari za uzima, natumai upo salama na unaenderea na majukumu ya kupambana na kazi ya kukufikisha kwenye ndoto zako.

Ndugu yangu nimeamua kuandika barua hii kwa wanafunzi pamoja na wahitimu wa masomo ya  ualimu sayansi pamoja na hisabati, ili kuweka sawa mambo kadha wa kadha.

Ni ukweli usio itaji mjadala kwamba Tanzania ya viwanda inaitaji wingi wa wataalamu wa sayansi katika sehemu tofauti tofauti, na ili tupate wataalamu hao hakuna budi kuwaitaji walimu wa masomo hayo ya sayansi, kwahiyo hizi na habari njema kwa wataaluma wa masomo hayo.

Lakini leo nimejikuta  naitafakari kwa  kina fani hii kwa miaka mitano iliyopita na kisha nikaitafakari kwa  miaka mitatu ijayo nikagundua kwamba  kadi miaka inavyo ongezeka fani hii inakuwa na changamoto za kutosha.

Nikagundua kwamba moja ya changamoto miaka mitano iliyopita kulikuwa na uhitaji wa walimu katika shule nyingi kutokana na sera ya nchi kuanzisha shule kila kata kutokana na sera hiyo basi ikapaswa kuweka hamasa  kwa wanafunzi kwenda kusoma kozi hiyo.

Lakini nikagundua kuwa baada ya miaka mitatu mbele kuna hali ya hatari kwa wahitimu wa masomo hayo maana  idadi yao imekuwa ni kubwa kuliko idadi ya shule, sijasema kwamba shule haziitaji walimu wa masomo hayo hapana, bali na maanisha kwamba ebu na wewe tafakari idadi ya wahitimu wanaomaliza na wanaoendelea kusomea na waliokwisha maliza na idadi za shule utaelewa na maanisha niini.

Kwahiyo ndugu yangu mhitimu huu si muda wa kusubiri ajira si muda wakujipa tumaini kwamba mwaka ujao utaajiriwa maana kila mwaka kuna idadi ya wahitimu wengi  mtaani kwahiyo wewe kusubiri miaka miwili ya ajira ni mara mia ungelianza kufuga kuku wawili kwa miaka miwili ungelikuwa ni mtaalamu wa kuku na ungelikuwa unajipatia kipato.

Kalamu naweka chini kwa kuhitimisha baua hii kwa kukuambia kwamba kama upo mtaani ebu toa mawazo kuhusu ajira kutoka serikalini kwanza, na kama upo shule ebu fikiria na kuhusu mtaani na baada ya hapo panga malengo yako na mikakati ya kuifikia kule unakotaka  kufika.

Asante sana kwa kusoma baua  hii nakukaribisha kwa maoni ushaui na changamoto inayokukabili nitumie email name nitakushauri.

Karibu sana

Aidan Mponeza
0762679204
aidanmponeza@gmail.com

No comments

Powered by Blogger.