HUYU NDO ADUI MKUBWA WA KUJIAMINI KWAKO.
Ndugu yangu hongera sana kwa siku ya leo hii ndio fursa pekee
ambayo inaweza kukufanikisha kufikia malengo yako maana hakuna fursa iliyokuu Zaidi
ya fursa ya uhai.
Uwezi kufika malengo yako kama aujiamini na kwa sababu hiyo
leo mtandao wa fikia lengo umekuletea Makala itakayokuonesha adui mkubwa wa
kujiamini kwako kabla sijaendelea na Makala hii nakushauri kuwa mwanachama wa
mtandao huu kwa kujiunga kupitia fomu iliopo katika mtandao huu.
Ndugu yangu uwezi kufanikiwa kama unao uwezo mdogo wa
kujiamini maana kama haujiamini auwezi kufanya vitu vikubwa vilivyo juu ya
uwezo wako.
Na kwa kawaida malengo yako makubwa kwa sasa yapo juu ya
uwezo wako na ndio maana unayafukuzia kuyashika
kwahiyo kama haujiamini basi upo kwenye hatari kubwa ya kutokutimiza
malengo yako.
Lakini ndugu yangu kama ulishawahi kutokewa na hali ya
kutojiamini juu ya kutekeleza jambo Fulani basi kuna adui mkubwa anae fanya
zoezi hilo.
Ndugu yangu hakuna adui mkubwa wa kujiamini kwako kama hofu,
hofu ndo adui anaekuambia uwezi pale unapoona ya kuwa unaweza, hofu ndo adui
anae kupa majibu hasi kabla hata ujafanya jambo Fulani.
Namna moja tu ya kumpinga adui hofu kwanza ni
kutokumsikiliza sababu zake maana sababu nyingi uwa ni za uongo unaweza ukawa
unataka kufika ofisi Fulani ukikaribia mlangoni utasikia hofu anakupa sabab ya
kutosafisha kiatu kuna nafsi utasikia ikisema “TAZAMA KIATU KILIVYO KICHAFU” huyo ndo adui hofu.
Lakini pia unaweza kumuepuka adui hofu na kuongeza uwezo mkubwa
ya kujiamini kwa kufanya maandalizi mazuri kabla ya tukio, maandalizi
humkimbiza hofu maana unakuwa umevunja sababu ambazo adui hofu uzitoa.
Ndugu yangu kwa leo mwandishi wako AIDAN MPONEZA naomba
niishie hapo tukutane kwenye Makala nyingine ndani ya mtandao huu lakini pia
katika mitandao yangu ya kijamii facebook page(FIKIA LENGO)
instagram@aidan_mponeza. Asante sana nakutakia mafanikio mema kwenye kazi zako.
instagram@aidan_mponeza. Asante sana nakutakia mafanikio mema kwenye kazi zako.
Leave a Comment