CHOCHOTE UNACHOKIFANYA UNAKIFANYA KWA HISIA HIZI.



Ndugu yangu habari za uzima.!

Kama kuna zawadi ambayo unastahili sana kujivunia kuwa nayo ni pamoja na zawadi ya siku ya leo hakuna zawadi kama hii maana msingi wa mafanikio yako yote yanatokana na siku hii ya leo kiukweli ni jambo la kumshukuru mungu.

Ndugu yangu karibu katika Makala ya leo ambayo itakwenda kueleza ni hisia zipi zinazo mfanya mtu kufanya kitendo chochote katika maisha yake, na kati ya hisia hizo ni ipi ni hisia sahihi kutumia.?

Ndugu yangu kama unafanya jambo lolote katika maisha yako basi elewa unafanya jambo hilo ukiongozwa na hisia kuu mbili katika kutimiza kufanya jambo hilo, zifuatazo ni hisia mtu atumiazo kufanya jambo au kitendo chochote chenye matokeo katika maisha yake.

Kwanza(HISIA YA HOFU); hofu ni moja ya hisia ambazo upelekea mtu kufanya jambo Fulani kwa mfano unaweza kutoa mchango Fulani labda wa harusi au msiba kwa kuhofia kuchekwa au kutengwa, na pia hisia hii ya hofu ndo inayopelekea mtu kutekeleza sheria zilizowekwa kwa kuhofia kukumbwa na adhabu kwa kukeuka sheria hizo. lakini sio kila tendo linafanywa kwa hisia hii ya hofu hapana.

Pili(HISIA YA MATAMANIO); hisia ya matamanio ni miongoni mwa hisia ambazo umtawala mtu katika kutekeleza jambo Fulani, mfano kama wewe unandoto za kuwa miongoni mwa mamilionea ndani ya nchi hii kwahiyo itakuitaji uwekeze, kitendo cha wewe kuwekeza uletwa na hisia tosha za matamanio ya kufika kule unataka.

JE IPI NI HISIA SAHIHI KUTUMIA; kiukweli ni kwamba hisia zote hizi mbili ni nzuri kutumia kutokana na jambo unalofanya lakini katika safari yako ya mafanikio ni vizuri ukatumia hisia ya matamanio Zaidi kuliko kutumia hisia ya hofu kwa maana kwamba hisia ya hofu uzalisha uwoga juu ya jambo ambalo unataraji kutekeleza sasa hii ni hatari kama hisia ya hofu ikikuzidia maana uwoga ni chanzo cha kutokujiamini.

Lakini ili ufike ni lazima utumie hisia zote hizi, ni lazima uwe na hisia ya matamanio makubwa ya kufika kule unataka na ni lazima pia uwe na hofu ya kupoteza kile ulichokipata ili uweze kufika salama.

Asante sana kwa Makala hii ya leo usiache kujaza taarifa katika mtandao huu ili uweze kupata Makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.
Aidan Mponeza
0762679204

No comments

Powered by Blogger.