BARUA YA WAZI KWA WATANZANIA JUU YA WASOMI WETU. 2017/2018
Ndugu yangu ni mimi mwandishi wako Aidan mponeza naandika
barua hii kwa mapenzi ya dhati na taifa langu na kwa Imani yangu naomba
iwafikie watanzania wote na wadau wa elimu ndani ya taifa hili. Kama
walimu,wazazi,madaktari na maprofesa na
wengine wengi.
ndugu ni hali ya kufurahisha na
kujipongeza kuona nchi yetu ilipofikia kwenye kiwango cha kuithamini elimu ni
hatua kubwa ambayo ni ya kujisifia lakini pia ni jambo la kujisifia taifa letu lilipo fikia
kwenye kiwango cha wazalishaji wasomi wengi kutoka vyuo vikuu mbalimbali ndani na
nje ya nchi ni jambo kubwa sana katika taifa.
Lakini pia jambo la kusikitisha ni kuona tunazalisha wasomi
ambao ni tegemezi kwa jamii badala ya jamii kuwa tegemea wao hili ni tatizo
katika taifa kama na mara nyingi tumekuwa tukirudisha mpira wa kona kwao wasomi
hao kwamba tatizo ni lao mimi leo nataka kuwatetea juu ya swala hili.
Ni sahihi wasomi kuwalaumu kwa hatua wanayopitia baada ya
kutoka vyuoni kwamba wao ndo tatizo hawachanganui akili zao lakini kuna tatizo
ambalo lipo nyuma ya pazia ambalo tusipo litatua tutakua tumepata janga la
kuzalisha wasomi waoga na wasiojiamini kwa kile walichosomea kuna ndugu yangu
mmoja nilimueleza kwamba tatizo la wasomi wengi kutokujiamini linatoka katika
jamii zetu kuanzia ngazi ya familia na akanibishia ila baada ya kumuelekeza akanielewa
vizuri sana.
Ukweli ni kwamba kama tukiendelea kuwashauri vijana wetu juu
ya kitu ca kuwasomea na kuwaambia kwamba kasomee kitu fulan tukubaliane na tatizo hili liendelee kutafuna
taifa.
Ukweli ni kwamba thamani ya elimu leo inabadilika kwa kasi
sana si muda wa kuipigia debe fani Fulani kwamba ni nzuri kwa ajira na
kuwashauri vijana wetu kwenda kuisoma ni kuzalisha kundi la waoga wa kitu
alichosemea maana utamshauri leo kwamba kasomee uandisi wa majengo kwamba ni
mzuri lakini kuja akamaliza miaka mine ya usomi wake anakuta thamani ya uandisi
wake umeisha hapo ndo anapunguza kutokujiamini juu ya alichosomea.
Ndugu yangu suluhisho la tatizo hili ni moja tu ili tuzalishe
wasomi wanaojiamini tukubaliane kwamba ni lazima tubadilishe ufundi wa kushauri
watoto juu ya elimu tunatakiwa kuwashauri watoto wetu kusoma wanachokipenda kwa
dhati na pia kuwashauri wasomi wetu hasa wa vyuo vikuu kuwa wasome
wanachokipenda na sio kisa baba upo kwenye nafasi Fulani unamshauri mwanao
kasome kitu Fulani utambeba elewa moja kwa moja unampoteza mtoto huyo kabisa.
"soma unachokiamini na kukipenda upate kujiamini na kupenda ulichosomea"AIDAN MPONEZA
Elewa kuwa mtoto akisoma anacho kipenda atapata nguvu kubwa
ya kukitetea kwa dhati maana kipo damuni kipo kwenye nafsi na ni tofauti na
yule anaesoma kisa pesa hizo zilikuwa ni zama za nyuma maana utasoma kisa kazi
yake inamshahara mkubwa je ukikosa kazi utapungukiwa hali ya kujiamini.
mwandishi AIDAN MPONEZA
simu no 0762679204kwa ushauri wowote juu kupitia mtandao huu BONYEZA HAPA
mwandishi AIDAN MPONEZA
simu no 0762679204kwa ushauri wowote juu kupitia mtandao huu BONYEZA HAPA

Leave a Comment